Skip to main content Accessibility help
×
Hostname: page-component-55f67697df-xq6d9 Total loading time: 0 Render date: 2025-05-10T06:41:39.466Z Has data issue: false hasContentIssue false

39 - Utii

Published online by Cambridge University Press:  17 April 2025

Get access

Summary

  • 1. Utii ni amri moja katika amri kubwa

  • 2. Utii wa mwili na akili

  • 3. Utii mapema katika utoto

  • 4. Kazi, skuli au jeshi huchafuka bila utii

  • 5. Katika maisha ya raia na utawala

  • 6. Huua tofauti, huleta uchovu

Utii ni amri moja katika amri kubwa za Mungu, tena amri yenyewe ina maana kubwa kabisa. Adamu na Hawa walitakiwa kutii. Hapana ujinga mkubwa katika maisha kama kufikiri kwamba mtu aweza kuishi bila utii wowote.

Kwa ajili ya kuendesha vema sheria au maisha lazima pawe na utii. Utii ni kazi ya kudumisha amri mahali pa machafuko. Kuna utii wa mwili na wa akili. Mwili ulioadabishwa, kama askari, hutii amri kama mashine. Akili iliyoadabishwa haishikwi na hasira ghafula. Hatuwezi kufunzwa utii na wengine siku zote. Lazima tujifunze sisi wenyewe.

Utii ndiyo njia bora ya kuweka msingi kwa ubora kwa wakati ujao wa mtoto. Lazima afunzwe kutii wazee na walimu wake, kuamka na kulala bila kuchelewa, kujifunza masomo yake na kutakasa mwili wake. Kuna wazee waharibuo watoto kwa kuwaruhusu kutenda lolote wapendalo kwa sababu ya mapenzi. Wadhani kwamba utii ni utumwa, namna ya neno litazamiwalo kwa watumishi. Lakini si utumwa. Ni adili ya kutengeneza uhuru wa mtoto. Mtoto asiyeadabishwa atakuwa mtu mwenye fujo ya mawazo na matendo ya ujinga.

Utii una maana kubwa sana katika madaraka au sheria. Kazi ambayo watumishi wake huja wakatoka wakati wowote wapendao, itajiona katika orodha ya kufilisika mara moja. Skuli, ambayo walimu na wanafunzi huja wakati wowote wapendao, yachekesha sana kufikiri. Utii si udhalimu. Jeshi bila utii huwa kama kundi la watoto watukutu. Hadithi hutwambia kwamba jeshi la askari milioni moja wasioadabishwa hushindwa upesi na jeshi la askari elfu tano walioadabishwa. Kwa hivyo, utii ni sehemu kubwa ya mafundisho ya jeshi. Kosa dogo la utii huadhibiwa kwa ukali.

Katika maisha ya raia na utawala wa nchi, utii hufaa sana. Serikali huongoza utawala kwa msaada wa kikosi kidogo sana cha polisi au askari. Lakini hufaulu, kwa sababu ya utii. Toka kwa Gavana mpaka kwa mtumishi mdogo kabisa, kila mtu hutii amri, lao si kuuliza kwa nini, ila ikipasa, kutenda au kufa. Kwa hivi utii hupasa kwa serikali. Hupasa vile vile kwa kila jamii ya watu.

Type
Chapter
Information
Kielezo cha Insha , pp. 75 - 76
Publisher: Wits University Press
Print publication year: 2024

Access options

Get access to the full version of this content by using one of the access options below. (Log in options will check for institutional or personal access. Content may require purchase if you do not have access.)

Save book to Kindle

To save this book to your Kindle, first ensure [email protected] is added to your Approved Personal Document E-mail List under your Personal Document Settings on the Manage Your Content and Devices page of your Amazon account. Then enter the ‘name’ part of your Kindle email address below. Find out more about saving to your Kindle.

Note you can select to save to either the @free.kindle.com or @kindle.com variations. ‘@free.kindle.com’ emails are free but can only be saved to your device when it is connected to wi-fi. ‘@kindle.com’ emails can be delivered even when you are not connected to wi-fi, but note that service fees apply.

Find out more about the Kindle Personal Document Service.

Available formats
×

Save book to Dropbox

To save content items to your account, please confirm that you agree to abide by our usage policies. If this is the first time you use this feature, you will be asked to authorise Cambridge Core to connect with your account. Find out more about saving content to Dropbox.

Available formats
×

Save book to Google Drive

To save content items to your account, please confirm that you agree to abide by our usage policies. If this is the first time you use this feature, you will be asked to authorise Cambridge Core to connect with your account. Find out more about saving content to Google Drive.

Available formats
×