Published online by Cambridge University Press: 17 April 2025
1. Uvumbuzi uwezeshao kusema na wote
2. Matumizi yake ya zamani
3. Maongozi na nguvu yake katika maisha
4. Mvuto wa elimu
5. Magazeti na vitabu
6. Hutuondolea giza kukatupa nuru
Kuandika kwa chapa ni uvumbuzi uwezeshao mtu yeyote kusema na umati mzima juu ya neno afikirilo kuwa muhimu, na uwezeshao nchi nzima kusikiliza maneno ya mtu kama huyo, kadiri alivyo mkubwa au mdogo, kwa urahisi na makini makubwa ya kuelewa asemayo kuliko mtawala Mwafrika anavyohutubia kabila katika baraza yake. Hatibu aweza kusema na watu waliopo, lakini kitabu kilichopigwa chapa hakisemi na kabila liliopo tu, ila husema na vizazi vyote vinavyofuata kikampatia na sifa mwandishi wake.
Tarehe ya kuvumbuliwa kuandika kwa chapa haijulikani hasa, lakini ikikadiriwa huwezekana kusemwa kwamba ni uvumbuizi wa karne ya kumi na tano. Caxton aliyeanzisha kiwanda chake mwenyewe cha kuandika kwa chapa akapiga chapa vitabu, husemwa kwamba ndiye mvumbuzi wa kuandika kwa chapa. Kuandika kwa chapa katika zama za kwanza kulikuwa si kwepesi wala hakukuwa wazi. Lakini kuandika kwa chapa kwa sasa ni ajabu ya kazi ya mashine.
Uvumbuzi wa kuandika kwa chapa umefanya maongozi makubwa sana katika hali zote za maisha. Kwa neno zima, uvumbuzi huu umeleta mageuzi makubwa kabisa katika ulimwengu. Kuandika kwa chapa ni uti wa malezi na elimu ya sasa. Hata katika karne ya kumi na tano uvumbuzi huu uligeuza maisha ya dini na nchi, kwa kufanya watu kujisomea wenyewe, badala ya kutengemea mashehe. Hivyo haki ya mashehe ya kumiliki elimu yote peke yao ilitanguka elimu ikawa miliki ya kila mtu.
Kuandika kwa chapa kulileta ufufuo wa elimu Ulaya. Zamani vitabu viliandikwa vikatunzwa katika miswada. Nakala nyingine zilipotakiwa, mtu ilimpasa kunakili kitabu kizima kwa mkono. Lakini kwa majilio ya kuandika kwa chapa idadi yoyote ya nakala huwezekana kupigwa chapa, na thamani ni ndogo. Maskini waweza kununua vitabu watakavyo. Elimu husafiri kila mlango. Maandiko huwa rahisi. Wakati na nguvu itumiwayo katika kunakili vitabu huokoka. Kwa hiyo kuandika kwa chapa kumesaidia sana maendeleo ya elimu.
To save this book to your Kindle, first ensure [email protected] is added to your Approved Personal Document E-mail List under your Personal Document Settings on the Manage Your Content and Devices page of your Amazon account. Then enter the ‘name’ part of your Kindle email address below. Find out more about saving to your Kindle.
Note you can select to save to either the @free.kindle.com or @kindle.com variations. ‘@free.kindle.com’ emails are free but can only be saved to your device when it is connected to wi-fi. ‘@kindle.com’ emails can be delivered even when you are not connected to wi-fi, but note that service fees apply.
Find out more about the Kindle Personal Document Service.
To save content items to your account, please confirm that you agree to abide by our usage policies. If this is the first time you use this feature, you will be asked to authorise Cambridge Core to connect with your account. Find out more about saving content to Dropbox.
To save content items to your account, please confirm that you agree to abide by our usage policies. If this is the first time you use this feature, you will be asked to authorise Cambridge Core to connect with your account. Find out more about saving content to Google Drive.